April 15, 2014

PATRICK YONDANI

Patrick Yondani, baba mzazi wa beki wa Yanga, Kelvin Yondani amesema mwanaye aachwe acheze mpira.

Yondani amesema mwanaye ana uwezo wa kufanya vizuri majukumu yake kama akiaminiwa na asingependa kuona anaingizwa matatizoni kwa mambo ya hisia.
BABA YONDANI AKIWA NA SALEH ALLY

“Unajua kwa anayejua mpira anaweza kujua mengi kwamba kuna kukosea na vingine. Lakini wako wasiojua na wenyewe wanalaumu kila jambo la kwenye soka.
“Sasa wamuache Kelvin acheze mpira, ameisharudi na ameungana na wenzake na umeona, amecheza vizuri mechi moja ile ya Arusha.
KELVIN YONDANI AKIWA NA KASEJA

Hivi karibuni, Yondani alishutumiwa na mashabiki kuhusiana na kufanya uzembe hadi Yanga kufungwa bao la pili dhidi ya Mgambo katika mechi Yanga waliyolala kwa mabao 2-1.
Baada ya hapo, beki huyo alipotelea kusikojulikana hadi alipoibuka wakati Yanga ikiondoka jijini Dar es Salaam kwenda Arusha kuivaa JKT Oljoro na kuishinda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic