Beki na nahodha
wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amewaambia
mashabiki na wapenzi wa timu yake kuwa, wasiwe na wasiwasi juu ya mechi ya
kesho Jumamosi dhidi ya Simba kwa kudai
kuwa kikosi chao kipo vizuri zaidi ya wapinzani wao hao na ana uhakika
watashinda kwa mabao mengi.
Timu hizo
zinatarajiwa kukutana katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa
ambapo mechi ya awali ya ligi hiyo matokeo yalisomeka 3-3, licha ya Yanga
kuongoza kwa mabao 3-0 mpaka mapumziko.
Cannavaro amesema wachezaji wamejipanga vizuri kuhakikisha
wanaibuka na ushindi mkubwa, licha ya kukosa ubingwa na kudai kuwa nia ni kulipa
kile kipigo cha mabao 5-0 ambacho Yanga ilifungwa mwaka juzi.
Beki huyo
mkongwe ameongeza kuwa, kipigo cha mabao matano walichokipata kipindi kile
kimekuwa kikiwaumiza mpaka leo licha ya kuwa ni muda mrefu umepita.
“Kushinda mechi
ya Jumamosi ndiyo kitu muhimu sana na lazima tulipize kipigo cha mabao matano
ambayo tuliwahi kufungwa na watani wetu na nawaahidi mashabiki wetu tutawapa
furaha baada ya kukosa ubingwa,” alisema Cannavaro kwa kujiamini.
0 COMMENTS:
Post a Comment