Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amewaambia mashabiki
wa timu yake wasiwe na hofu na wajitokeze kwa wingi.
Logarusic amesema mashabiki watakaokwenda Uwanja wa Taifa
jiini Dar, leo watawaona Yanga wakiteseka.
“Najua watacheza kwa kasia na kukimbia sana, lakini mje muone
wanavyoteseka. Waambie mashabiki wasiwe na hofu,” alisema mara tu baada ya
Simba kutua ikitokea Zanzibar, jana jioni.
Yanga na Simba zinacheza mchezo wa kufunga ligi leo kwenye
uwanja huo.
0 COMMENTS:
Post a Comment