April 15, 2014


Pamoja na kulipwa mamilioni ya fedha na klabu yake ya Arsenal, mshambuliaji Lukas Podolski ameonyesha hana makuu na anapenda maisha simpo.


Mjerumani huyo nyota pia wa timu yake ya taifa, ameonekana akikwea daladala za mji wa London kama kawa.
Jana asubuhi, Podolski alipanda basi No 26 linalokwenda kutoka Hackney Wick likikatiza maeneo mbalimbali ya jiji la London hadi stesheni ya Waterloo.
Si kawaida kwa wachezaji nyota na hasa wa timu zinazoshiriki Ligi Kuu England kupanda mabasi.
Katika moja ya picha, utaona Mjerumani huyo akizozana na shabiki aliyetaka wapige picha wakati yeye alionyesha ana haraka.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic