Mshambuliaji Emmanuel Okwi hataichezea
Yanga tena msimu huu baada ya kocha Hans van Der Pluijm kumtema rasmi.
Kutokana na uamuzi wa kocha huyo, maana
yake Okwi ataikosa mechi ya kufunga ligi kuu dhidi ya wapinzani wao Simba, keshokutwa.
Pluijm raia wa Uholanzi, amemuacha OKwi
katika kikosi chake kilichoweka kambi kwenye hoteli ya Bahari Beach jijini Dar es
Salaam baada tu ya kurejea ikitokea Arusha.
Habari kutoka ndani ya Yanga zimeeleza,
kocha huyo alihimiza Okwi aingie kambini kabla hawajaenda kambini kwenda
Arusha, la sivyo hapampa nafasi ya kucheza.
Lakini baadaye Kocha wa Makipa wa Yanga,
Juma Pondamali akaongeza kuwa kweli Okwi pamoja na Niyonzima hawataivaa Simba,
Jumamosi.
“Niyonzima ni mgonjwa kama ilivyo kwa
Bahanuzi ambaye anaumwa malaria lakini Okwi hakuingia kambini tokea tunakwenda
Arusha, kocha kasema haitakuwa sahihi. Hivyo hatakuwepo.
"Mwingine ambaye hatakuwepo ni Kaseja ambaye pia hakuwepo kambini,” alisema.
Okwi amekuwa akiweka mgomo kwa kuwa
anaidai Yanga dola 40,000 ambazo hajamalizia kwenye usajili wake uliogharimu
dola 100,000.
0 COMMENTS:
Post a Comment