Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Salum Mayanga ametangaza wachezaji wengine 23
watakaoingia kambini kesho (Aprili 20 mwaka huu) kuungana na 16 waliotajwa
awali kujiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Burundi itakayochezwa Aprili 26
mwaka huu.
Katika waliotajwa, wachezaji watano
wa safu ya ulinzi wametokea katika kikosi cha mabingwa Tanzania Bara, Azam FC.
Wachezaji walioitwa ni makipa Aishi
Manula (Azam), Deogratias Munishi (Yanga) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni Abdi
Banda (Coastal Union), Aidan Michael (Ruvu Shooting), Aggrey Morris (Azam),
Erasto Nyoni (Azam), Hassan Mwasapili (Mbeya City), Kelvin Yondani na Said
Moradi (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Frank
Domayo (Yanga), Himid Mao (Azam) na Jonas Mkude (Simba).
Washambuliaji ni Athanas Mdamu
(Alliance), Haruna Chanongo (Simba), Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Khamis Mcha
(Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngasa (Yanga), Mwinyi Kazimoto
(Markhiya, Qatar), Ramadhan Singano (Simba), Simon Msuva (Yanga) na Thomas
Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).
Wachezaji walioitwa kutoka katika
kikosi cha maboresho ni kipa Benedicto Tinoko Mlekwa (Mara), mabeki wa kati;
Emma Namwondo Simwanda (Temeke) na Joram Nason Mgeveje (Iringa). Walinzi wa
pembeni ni Omari Ally Kindamba (Temeke), Edward Peter Mayunga (Kaskazini Pemba)
na Shiraz Abdallah Sozigwa (Ilala).
Viungo ni Yusuf Suleiman Mlipili
(Temeke), Said Juma Ally (Mjini Magharibi), Abubakar Ally Mohamed (Kusini
Unguja), Hashim Ramadhan Magona (Shinyanga), Omari Athumani Nyenje (Mtwara) na
Chunga Said Zito (Manyara).
Washambuliaji ni Mohammed Seif Saidi (Kusini Pemba), Ayoub Kasim Lipati (Ilala), Abdurahman Othman Ally (Mjini
Magharibi), Paul
Michael Bundara (Ilala). Wachezaji wa U 20 ni Mbwana
Mshindo Musa (Tanga) na Bayaga
Athanas Fabian (Mbeya).
Taifa Stars inayodhaminiwa na
Kilimanjaro Premium Lager itaingia kambini kwenye hoteli ya Kunduchi Beach.
0 COMMENTS:
Post a Comment