April 15, 2014


Mshambuliaji nyota wa Simba, Amissi Tambwe amesema anataka kufunga angalau bao moja katika mechi dhidi ya Yanga, Jumamosi.

Tambwe amesema kwa kuwa wamekosa ubingwa na nafasi ya pili, anaamini mashabiki wao watakuwa na furaha kubwa kuwaona wanashinda mechi hiyo.
“Pia ningependa kufunga bao moja au zaidi kutokana na mchezo utakavyokuwa.
“Napenda kuwafunga Yanga, lakini napenda kuona timu yangu ya Simba inashinda mechi hiyo ya watani,” alisema Tambwe.
Tambwe anaongoza listi ya wafungaji bora akiwa na idadi ya mabao 19.
Idadi hiyo tayari imevuka ile ya mfungaji bora msimu uliopita, Kipre Tchetche raia wa Ivory Coast.

Mechi hiyo ya Jumamosi itakuwa ni funga dimba Ligi Kuu Bara huku Yanga ikiwa na uhakika wa kushina nafasi ya pili, wakati watani wao wanagombea kubaki katika nafasi ya nne.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic