April 16, 2014

HALL (KUSHOTO) WAKATI AKIWA AZAM

Viongozi na wachezaji wa timu ya Azam FC wametoa shukrani kwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Stewart Hall, kwa kuchangia mafanikio ya timu hiyo na kuweza kuibuka mabingwa wa Ligi Kuu Bara.


Hall aliifundisha timu hiyo katika mzunguko wa kwanza na mpaka anaiacha ilikuwa haijawahi kupoteza mchezo.

Akizungumza na Championi Jumatano, Hall alisema amefurahi kwa kiasi kikubwa timu hiyo kuweza kuleta mabadiliko huku wachezaji pamoja na viongozi wa timu wakiwa wamempigia simu kumshukuru kwa mchango wake.

Stewart alisema mabadiliko yaliyotokea safari hii katika soka ni mazuri na ndiyo yatafanya soka la Tanzania kuendelea kukua kwa kiasi kikubwa kutokana na changamoto na zama za Simba na Yanga huenda zikatoweka.

“Nina furaha sana kutokana na Azam kutwaa ubingwa msimu huu, haya ndiyo mabadiliko tuliyokuwa tunayahitaji na nimepata meseji za shukrani kutoka kwa viongozi kama Bakhresa, Kali Ongalla na wengine wengi.

“Lakini kikubwa hapa ni mabadiliko kwa kiasi kikubwa, msimu huu tumeona changamoto nyingi sana kutoka kwa timu nyingi ili kumaliza zama za Simba na Yanga. Kwa sasa wanasoka wameamua kuleta mabadiliko makubwa, tofauti na zamani,” alisema Hall.
SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic