July 27, 2014


Klabu ya Al Shaolla ya Saudi Arabia imeamua kusitisha mkataba wake na makocha Hans van der Pluijm raia wa Uholanzi na Charles Boniface Mkwasa, Mtanzania.
Habari za uhakika kutoka Saudi Arabia zimeeleza kumetokea hali ya kutoelewana kati ya makocha hao na uongozi.

SALEHJEMBE, imefanya juhudi za kuwasaka wawili hao hadi ilipompata Mkwasa ambaye ametoa ufafanuzi.
Mkwasa amesema tatizo lililosababisha wao  kuingia kwenye mzozo ni suala la usajili.
“Kweli hapa hali imebadilika ghafla baada ya kocha na uongozi kushindwa kuelewana kutokana na usajili wa wachezaji wapya kwa msimu ujao.
Viongozi waliwaleta wachezaji kwa majaribio ambao kwa muono wa kawaida hawakuwa na uwezo mzuri.
“Kwa ujumla tuliwakataa na pia walikuwa wanataka wachezaji kutoka madaraja ya chini pia walikataliwa, wao hawakupendezewa nalo hivyo wakaamua kusitisha mikataba yetu kwa sababu kubwa wanasema hawana fedha,” alisema Mkwasa na kuendelea kufafanua.

“Msimu uliopita timu hii ilishika nafasi ya 12 ambayo ni timu ya mwisho kubaki daraja hivyo coach Hans alitaka wasajili wachezaji wenye uwezo ili waweze kufanya uzuri, kama haitoshi wachezaji wachache wazuri wa Shoulla wa msimu uliopita nao walihama so timu ilikuwa inahitaji wachezaji wengi na wa hali ya juu.
“Habari ndiyo hiyo, likiharika lawama kwa kocha usajili wanataka wa chee.
Taratibu za safari ya kurudi makwetu zinafanyika.”
Pluijm ndiye alianza kujiunga na Shoulla kabla ya kumpendeleza Mkwasa ambaye alifanya naye kazi Yanga kwa ufasaha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic