July 30, 2014

SALEH (KULIA) AKIWA NA NGASSA WAKATI YANGA IKIJIFUA UFUKWENI CHINI YA KOCHA MARCIO MAXIMO.


Beki wa pembeni aliyetemwa Yanga hivi karibuni, Saleh Abdallah, ameibuka na kusema kuwa anaidai Yanga mamilioni ya shilingi ili kukamilisha taratibu za uvunjwaji wa mkataba wake klabuni hapo.
Saleh ambaye alisajiliwa na Yanga mara baada ya kumalizika kwa ligi kuu msimu uliopita akitokea Azam B, alifungashiwa virago wiki iliyopita na klabu hiyo, sababu kubwa ikielezwa kuwa ni kiwango duni.

Saleh ameiambia SALEHJEMBE hajaridhishwa na uvunjwaji wa mkataba wake na Yanga, hivyo bado ana haki zake za msingi kwa ajili ya kukamilika kwa zoezi hilo ikiwemo kulipwa ada yake ya usajili pamoja na mshahara wa miaka mitatu, ambapo alisema kuwa jumla yake ni zaidi ya Sh milioni 21.
“Unajua pale Yanga nilisajiliwa kwa mkataba wa miaka mitatu, sasa uongozi umeniambia tu kwamba nimevunjiwa mkataba wangu kwa kuwa kocha (Marcio Maximo) hajaridhika na uwezo wangu, sawa ila inabidi nipewe haki yangu kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kuvunja mkataba.
“Bado nafuatilia haki yangu, mkataba unajieleza kila kitu kwamba nini kifanyike kama ikitokea umevunjwa, nahitajika kwanza kumaliziwa ada yangu ya usajili na kulipwa mshahara wa misimu miwili iliyobaki ambayo kwa mahesabu ya haraka haraka ni zaidi ya milioni 21,” alisema Saleh aliyeng’ara na kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23, Ngorongoro Heroes, iliyotolewa na Nigeria katika kufuzu Fainali za Vijana Afrika.  
Hata hivyo, taarifa zaidi zinaeleza kuwa, tayari mchezaji huyo alishapewa kiasi cha shilingi milioni tano kama utangulizi wa ada ya usajili wake. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic