July 28, 2014


KIIZA (KUSHOTO)


Kocha Marcio Maximo sasa ndiye atakayeamua kuhusiana na Emmanuel Okwi na Hamis Kiiza, lakini baada ya kufanya nao kazi angalau kwa wiki moja.

Huenda wakaungana na Yanga jijini Dar es Salaam au mjini Pemba.
OKWI

Okwi na Kiiza wanalazimika kugombea nafasi moja ya wachezaji wa kimataifa iliyobaki.


Uongozi wa  wote wanatarajiwa kutua nchini ndani ya siku chache zijazo kuanza kazi na kocha mpya, Marcio Maximo, imefahamika.

Nafasi nyingine nne zimetwaliwa na Wabrazil, Jaja na Coutinho wakati mbili wamechukua Wanyarwanda, Mbuyu Twite na Haruna Niyonzima.

Uongozi wa Yanga umeamua kulikabidhi suala hilo kwa Maximo, ambaye mwisho ataamua kwamba abaki na Okwi au Kiiza.

“Kwa kuwa ameachiwa Maximo, yeye kama kocha ametaka wote waje kazini na mwisho ataamua yupi kati yao atakuwa anamhitaji kutokana na kikosi chake kinahitaji nini.

“Hivyo wote watakuja na kuungana na wenzao mara tu watakapomaliza majukumu ya kikosi cha timu yao ya taifa,” kilieleza chanzo cha uhakika.

Yanga imekuwa haijui imuache nani kati ya Okwi au Kiiza ili kumuachia nafasi Jaja, mshambuliaji mpya kutoka Brazil. Kwa mujibu wa Sheria za TFF, wachezaji wa kigeni wanatakiwa kuwa ni watano tu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic