SAID MECK SADIQ, MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM (KULIA) AKIWA NA MWENYEKITI WA KAMATI HIYO, FAROUK BAGHOZA (ANAYEMFUATIA), WENGINE NI WAJUMBE WA KAMATI HIYO, SAAD KAWEMBA NA HAGILA. |
Kamati inayoshughulikia ujio wa klabu
kongwe duniani ya Real Madrid, leo imetua kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiq na kupata baraka.
Mkuu huyo wa mkoa, amewatakia maandalizi
mema watu hao wa kamati.
“Kweli tumepata Baraka za mkuu wa mkoa
ambaye ndiye baba wa mkoa wetu. Ametupa Baraka tuendelee na maandalizi ambalo
ni jambo jema.
“Tumefurahi na nguvu ya kuendelea kufanya
jambo hilo imeongezeka, nyie mnasema morali. Hivyo tunaamini mambo yatakwenda
vizuri,” alisema Ssebo ambaye ni mratibu wa ziara hiyo.
Wakongwe hao wa Real Madrid wanatarajia
kutua nchini na kukipiga Agosti 23 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Ssebo alisema maandalizi yanaendelea vizuri na wanatarajia kupata sapoti ya Watanzania pamoja na makampuni kuhusiana na ugeni huo mkubwa wa kimichezo nchini.
Wachezaji nyota wa zamani wa Real Madrid
wanaoounda kikosi hicho wakiwemo Luis Figo na wenzake.
0 COMMENTS:
Post a Comment