Kipa wa Coastal Union, ShabanI Kado amejikuta akiacha gumzo kwenye
mitandao ya kijamii ya Instagram na Facebook baada ya kutupia picha
inayomuonyesha akitumia bunduki.
Kado alitupia picha hiyo kwenye kurasa zake zote mbili za mitandao
hiyo, ambapo picha moja ilionyesha akilenga ilipo kamera, ya pili alikuwa
ameishika bastola hiyo kulenga kichwa chake na ya tatu ni picha ya bastola
ikiwa juu ya meza.
Alipopigiwa simu kuhusiana na suala hilo, Kado alicheka
kisha akajibu: “Siyo yenyewe hiyo mwanangu, hilo pambo tu ila ukiitazama ni
kama ya ukweli, ipotezee kama vipi.”
0 COMMENTS:
Post a Comment