Kikosi cha Taifa
Stars, kinatarajiwa kuondoka nchini leo Jumatano, kuelekea Msumbiji lakini
kitaweka kambi ya muda mfupi Afrika Kusini ambapo kitaungana na washambuliaji
Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.
Stars inakwenda
Msumbiji kwenye mchezo wa marudiano wa kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za
Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Morocco mwakani.
Katika mchezo wa
kwanza uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa siku chache zilizopita, Stars ilijikuta
ikimaliza vibaya baada ya kuambulia sare ya mabao 2-2 na sasa itatakiwa
kuhakikisha inaibuka na ushindi au sare ya zaidi ya mabao hayo.
Katibu wa
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa, alisema timu hiyo
inatarajia kuondoka nchi leo Jumatano kwa ajili ya kuelekea nchini Msumbiji katika
mchezo huo wa Jumapili.
“Timu inatarajiwa kuondoka nchini leo
kuelekea Maputo Msumbiji kwa ajili ya mchezo wa marudiano ambao utachezwa siku
ya Jumapili, lakini itapumzika kidogo Afrika Kusini ambapo itaungana na Samatta
na Ulimwengu ambao wanacheza TP
Mazembe ya Congo.
“Kwa upande wa kikosi, wachezaji wote wapo
vizuri na jana wamefanya mazoezi kama kawaida, naamini kuwa tutaibuka na
ushindi kwenye mchezo huo,” alisema Mwesigwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment