July 25, 2014



Ushindani wa namba ndani ya kikosi cha Azam FC hasa kwenye safu ya ushambuliaji unazidi kuwa mkali ambapo sasa kila mmoja amejinadi kufanya vizuri ili kumshawishi kocha ampange katika kikosi cha kwanza.


Kipre Tchetche, raia wa Ivory Coast, amefunguka kuwa, hana hofu juu ya nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza lakini akaongeza kuwa, anafurahia ushindani kwa kuwa ni kwa faida ya timu yake.

Safu ya ushambuliaji ya Azam FC sasa inaundwa na Kipre, Didier Kavumbagu raia wa Burundi, Leonel Saint Preux wa Haiti na Watanzania John Bocco, Gaudence Mwaikimba na Kelvin Friday.

“Kuwepo kwa mastraika wengi katika kikosi chetu ni moja ya mafanikio na kuongeza ushindani, nitaendelea kujituma lakini naamini uwezo wangu upo juu.

“Lakini kikubwa ni kuwa tunajipanga vema kuhakikisha tunafanya vizuri, ujio wa wachezaji wapya ni mzuri na ujue kuwa hakuna mchezaji ambaye namhofia,” alijinadi Tchetche ambaye alishika nafasi ya pili kwa ufungaji katika Ligi Kuu Bara msimu uliopita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic