July 23, 2014



RASMI! mambo yamekamilika na sasa timu ya magwiji au wakongwe wa klabu ya Real Madrid ya Hispania itatua nchini Agosti 22, mwaka huu kwa ajili ya kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya kikosi maalum cha nyota wa Tanzania Agosti 23.

Magwiji hao wanaotarajiwa kuongozwa na Zinedine Zidane, Luis Figo, Ivan Helguera na wengine wengi watakuwa na ziara ya siku nne nchini ikiwa ni pamoja na kutembelea mkoani Arusha kwa ajili ya kutazama vivutio vya utalii.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam jana, meneja wa ziara hiyo, Denis Ssebo, amesema kwamba mpaka sasa ziara hiyo ina idadi ya watu 50, wakiwemo wachezaji wenyewe na viongozi wao 27 pamoja  na mashabiki 23 waliojitokeza kutaka kuongozana na mastaa hao lakini alisisitiza kuwa idadi inaweza kuongezeka kulingana na maombi ya mashabiki hao.
Aidha, aliongeza kuwa timu ya Tanzania itakayocheza na mastaa hao kwenye Uwanja wa Taifa itaundwa na wachezaji kutoka Taifa Stars, huku kocha wa kikosi hicho akiwa ni  Kocha Mkuu wa Stars, Mholanzi Mart Nooij.
“Kikosi cha magwiji au wakongwe wa Real Madrid kitatua rasmi Agosti 22, na kitakuwa na ziara ya siku nne ambapo Agosti 23, kitacheza mechi ya kirafiki dhidi ya kikosi maalum cha Tanzania kitakachokuwa chini ya kocha mkuu wa Stars.
“Baada ya hapo Agosti 24, wataelekea Arusha kwa ajili ya kujumuika pamoja na wakazi na mashabiki wa kuangalia vivutio mbalimbali vilivyopo mkoani humo.
“Baada ya hapo Agosti 26 watakwea pipa kurejea kwao, viingilio vya mechi hiyo bado havijatangazwa lakini itakuwa ni vya chini kwa ajili ya kumuwezesha kila Mtanzania kuushuhudia huo mtanange,” alisema Sssebo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic