Ungekuwa wewe ungevunga lakini si Cristian
Karembeu wa Real Madrid. Mara tu baada ya kumfikia Rais wa Tanzania, Jakaya
Mrisho Kikwete, fasta akaomba apewe ‘shavu’.
Karembeu ambaye alikuwa nchini na kikosi cha
wakiongwe cha Real Madrid, alimuomba Rais Kikwete wapige picha pamoja kutumia ‘tab’
yake.
Rais kwa kuwa ni mtu wa watu, wala
hgaikuchukua hata sekunde, akasogea na Karembeu akafyatua ‘ta, ta, ta’.
Picha hiyo kwa ajili ya kumbukumbu, Karembeu
ambaye kikosi chake siku hiyo kiliichapa Tanzania Eleven 3-1, anaweza kujidai
nazo Facebook, Twitter au Instagram.
0 COMMENTS:
Post a Comment