Kocha wa Brazil, Dunga ametangaza kikosi chake kwa
ajili ya ya mechi za kirafiki dhidi ya Colombia, mechi itakayopigwa Septemba 5
jijini Miami, na dhidi ya Ecuador Septemba 9 jijini New Jersey, Marekani.
Kati ya wachezaji aliowaita ni Miranda wa Atlético
de Madrid na Filipe Luís.
Lakini Dunga akaamua kuwaacha mabeki Dani Alves wa
Barcelona na Marcelo wa Real Madrid.
Nahodha Thiago Silva anayekipiga PSG pia ni
mgonjwa, hivyo pia amemuacha katika kikosi chake.
Wachezaji waliocheza Kombe la Dunia 2014 ambao Dunga
amewaita ni Jefferson, David Luiz, Maicon, Luiz Gustavo, Fernandinho, Ramires,
Oscar, Hulk, Willian and Neymar.
0 COMMENTS:
Post a Comment