MUSOTI (KUSHOTO) AKIWA MAZOEZINI AKIWA MAZOEZINI PAMOJA NA KISIGA. |
Huku muda wa kufunga usajili wa Ligi Kuu
Bara ukiwa unayoyoma kwenda ukingoni, Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri
ameachiwa zigo la kuchagua beki yupi abaki kikosini mwaka kati ya Donald Musoti
na Butoyi Hussein raia wa Burundi.
Musoti tayari amekuwa akijifua na Simba
lakini Butoyi kutoka Telecom ya Djibout.
Lakini uongozi wa Simba umeelezwa kumuachia
Patrick Phiri achukue uamuzi wa mwisho.
Simba sasa ina wachezaji sita wa kigeni,
wakati wanatakiwa watano tu.
Na nafasi moja wanatakiwa wawanie kati ya
Musoti na Butoyi ambaye ni raia wa Burundi.
0 COMMENTS:
Post a Comment