Kocha Marcio Maximo wa Yanga amesema
asingependa kumfanya mshambuliaji Emmanuel Okwi ndiyo ishu.
Okwi yuko jijini Dar es Salaam akiisubiri
Yanga ili ajiunge nayo.
“Unafikiri sawa nianze kujadili kuhusiana na
mchezaji mmoja.
“Nimesema mara ngapi sipendi kujadili
majina, hivyo tuachane na suala la Okwi.
“Vizuri tujadili Yanga kama timu inataka
kufanya nini,” alisema Maximo.
Yanga ipo kisiwani hapa ikiendelea kujifua
kwa ajili ya msimu ujao.
Okwi alichelewa kuja kambini kujiunga na
Yanga kwa madai kwamba hajalipwa fedha zake.
0 COMMENTS:
Post a Comment