Kocha Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog amewaita wachezaji wake kuanza
mazoezi kesho ili kumalizia maandalizi ya msimu mpya.
Meneja Azam FC, Jemedari Said amesema kikosi chake kitaanza mazoezi
kesho.
Wachezaji ambao hawakuwa kwenye kikosi cha timu ya taifa wataanza
mazoezi.
“Baada ya hapo, wale ambao walikuwa kwenye kikosi cha timu ya taifa,
pia wataungana na wenzao,” alisema Jemedari.
Omog alitoa mapumziko kwa wachezaji wake mara baada ya michuano ya
Kagame nchini Rwanda.
Azam FC ilitolewa kwenye michuano hiyo katika hatua ya robo fainali
dhidi ya El Merreikh ya Sudan ambayo ndiyo imeibuka na kuwa bingwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment