Kikosi cha Tanzania Eleven chini ya Kocha
Charles Boniface Mkwasa, kitaweka kambi kwenye hoteli maarufu ya kisasa ya Sapphire Court
ya jijini Dar es Salaam.
Kambi hiyo inatarajia kuanza kesho na wachezaji
wataingia kambini hapo kujiandaa kwa ajili ya mechi dhidi ya wakongwe wa Real
Madrid itakayopigwa jijini Dar es Salaam, Jumamosi.
Madrid itaongozwa na Luis Figo aliyewahi kuwa
nota wa Barcelona, baadaye Real Madrid na Inter Milan.
Mechi hiyo inasubiriwa kwa hamu na tayari
tiketi zimeanza kuuzwa katika sehemu mbalimbali.
0 COMMENTS:
Post a Comment