Pamoja na kuendelea kucheza soka nchini Sweden mshambuliaji
Athuman Machuppa ameamua kujiongezea kipato zaidi kwa kufanya kazi za kawaida.
Mtanzania, Machuppa ambaye aliwahi kung’ara akiwa Simba na timu ya
soka ya taifa, Taifa Stars sasa anafanya kazi kwenye Mhahawa mkubwa nchini humo
na duniani kote wa MacDonald.
“Kweli nacheza soka na pia nafanya kazi kaka, si unajua maisha ni
kujituma,” alisema Machuppa kutoka Stockholm.
Machuppa amekuwa akiishi nchini humo kwa zaidi ya miaka sita
akikipiga katika timu mbalimbali.
Wakati akiwa kinda, Machuppa alifahamika kwa kasi, ujuzi na
mashuti ya kushitukiza.
0 COMMENTS:
Post a Comment