September 2, 2014



Kikosi cha Mbeya City inayodhaminiwa Kampuni ya Bin Slum Tyre kinaonekana kupania kufanya vizuri zaidi msimu ujao baada ya kuweka kambi nje ya mji.
Msemaji wa Mbeya City, Dismas Ten amesema wanaendelea na maandalizi makubwa kwa kuwa wamepania kucheza michuano ya kimataifa.
“Tumeamua kuweka kambi nje ya mji wa Mbeya kwa ajili ya kujiimarisha zaidi na mwalimu Juma Mwambusi anaendelea na maandalizi.
“Lengo ni kucheza michuano ya kimataifa ukizingatia Mbeya City ni kati ya timu zinazotupiwa macho na wengi.
“Hivyo lazima kujiandaa vilivyo na tunataka kufanya vizuri ingawa tunajua si kazi lahisi,” alisema Dismas.
Mbeya City ilimaliza msimu uliopita ikiwa katika nafasi ya tatu nyuma ya mabingwa Azam FC na Yanga walioshika nafasi ya pili.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic