Mtibwa Sugar chini ya Mecky Maxime imeifunga kwa mabao 2-0 katika
mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara.
Yanga imelala ikiwa chini ya Marcio Maximo ambaye alikuwa mwalimu
wa Maxime wakati akiinoa Taifa Stars.
Katika mechi hiyo leo kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro huku
mashabiki wa Yanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi, timu yao ilitawala kipindi
cha kwanza tu.
Lakini ikashindwa kuonyesha cheche katika kipindi cha pili na
kulala kwa mabao 2-0.
Mabao ya Mtibwa Sugar yalifungwa na Mussa Hassan Mgosi katika
dakika ya 56 na dakika tatu baadaye Ame Ally akafunga la pili na kuimaliza
Yanga.
Juhudi za Yanga kutaka kusawazisha hazikuzaa matunda na Mtibwa
ndiyo walioonekana kukitawala kipindi cha pili.
0 COMMENTS:
Post a Comment