September 16, 2014

Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri amesema kamwe hajawahi kuonyesha dharau kwa Yanga kwamba ni timu lahisi.

Lakini akasisitiza, hakuwahi wala hataiogopa Yanga hata siku moja, badala yake atafuata misingi ya kazi yake.
Phiri raia wa Zambia ameiambia SALEHJEMBE kuwa, kocha makini hawezi kuhofia kitu, badala yake anajipanga.
“Dharau ni sehemu ya kutoka nje ya mfumo sahihi ya kocha bora.
“Kocha bora anajipanga kushinda na si kushindwa. Ukidharau maana yake unapotea na inaweza kuwa lahisi kushindwa.
“Yanga ni moja ya timu kubwa, kongwe na zenye mafanikio hapa Tanzania. Siwezi kuidharau hata kidogo.

“Badala yake ninaheshimu wanachofanya na tunapokaribia kukutana nao, najiandaa vizuri kutokana na ninavyowajua,” alisema Phiri ambaye alikuwa uwanjani wakati Yanga inaivaa Azam FC na kuichapa kwa mabao 3-0.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic