September 1, 2014


 Unaweza kudhani Louis van Gaal amelala na anasajili washambuliaji tu, la! Wakati dirisha la usajili linakwenda ukingoni kufungwa, Manchester United imemnasa beki kisiki wa Ajax, Daley Blind.

Blind anayeweza kucheza kama beki wa kushoto, beki wa kati au kiungo mkabaji ‘ameikost’ Man United pauni milioni 14.

Mkali huyo ambaye ni mwanasoka bora wa Uholanzi msimu uliopita akiwa na Ajax, pia alikuwa kwenye kikosi cha Uholanzi kilichoshika nafasi ya tatu kwenye Kombe la Dunia, kocha akiwa van Gaal.
Ilikuwa inaonekana wazi kwamba Man United ina tatizo kubwa kwenye ulinzi na sasa kocha huyo atakuwa amelipatia ufumbuzi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic