September 2, 2014



MAMA KARUME (KUSHOTO) NA KIMEI WAKIINGIA MKATABA KWA NIABA YA YANGA NA CRDB.

Klabu kongwe nchini ya Yanga, imeingia mkataba wa kudumu na Benki maarufu nchini ya CRDB.
CRDB ndiyo itakayofanya kazi ya kutengeneza kadi za wanachama wa Yanga ambao watakuwa wakikatwa ada zao moja kwa moja.
Kabla, Yanga ilikuwa na mkataba na Benki ya Posta (TPB) ambayo ilikuwa ikiendesha kampeni za kuingiza wanachama wapya.

Maana yake sasa, benki ya Posta imebaki na watani wa Yanga, Simba ambao wanaendelea nayo.
Lakini leo wakati wa uingiaji mkataba ulioongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Yanga, Mama Fatma Karume na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa CRDB, Charles Kimei, suala la TPB halikutakiwa kugusiwa.
Kimei amesema kuwa makubaliano hayo waliyoingia siyo ya kushindana na benki nyingine yoyote kikubwa ni kuwafikia wanachama karibu.
Kimei alisema, wanachama wa timu hiyo wanatakiwa kuchangia kiasi cha shilingi 8000 kwa ajili ya kufungulia akaunti huku kadi ikitolewa bure bila ya malipo yoyote.
 “Sisi tutakuwa tayari kuwapa nafasi hata wale wenye klabu nyingine, lakini kwa kuwa tumeingia mkataba na Yanga, tunawapa kipaumbele zaidi,” alisema Kimei.
 “Mkataba wetu hauna kikomo ni wa muda mrefu, wao au sisi mmoja wao kama hasiporidhishwa na huduma ya mwenzake, atasitisha mkataba,”alisema Kimei.
Kuhusiana na mkataba huo alioingia mbele ya waandishi, Mama  Karume alisema kuwa wanaamini utakuwa na mafanikio makubwa.

“Tunaishukuru benki ya CRDB ya kuingia mkataba na Yanga huu wa utengenezaji wa kadi za uanachama huku tukipata huduma za kibenki.
“Nafikiri hiyo ni kutokana na uongozi bora wenye busara uliokuwepo madarakani, Yanga hivi sasa ni klabu kubwa yenye kiwango cha kimataifa, hivyo inahitaji kupata wadhamini zaidi ya hapa ilipofikia,”alisema Karume.
CRDB ni kati ya benki kubwa zaidi nchini zilizosambaa nchi nzima, hali ambayo itaisaidia Yanga kupata wanachama kwa wingi zaidi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic