September 2, 2014



Kuna taarifa kuwa Yanga imemalizana na Benki ya CRDB na huenda leo wakaingia mkataba wa awali.
Taarifa za uhakika zimeeleza kuwa Yanga imeamua kuachana na Benki ya Posta (TPB) ambayo iliingia nayo mkataba sambamba na klabu ya Simba pia.
Lakini Yanga imeamua kujiengua na kutafuta wadhamini wapya huku ikifanikiwa kuwapata CRDB.
“Kweli Yanga wanaingia mkataba na CRDB na tumeambiwa kuwa wameishafanya utaratibu wa kuvunja mkataba na TPB,” kilieleza chanzo.
Viongozi wote wa Yanga, hawakutaka kulizungumzia suala hilo huku wakisisitiza utafanyika mkutano wa waandishi leo na mambo yote yatawekwa hadharani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic