Zinedine Zidane huenda
akafungikiwa kufundisha soka barani Ulaya kwa miezi sita.
Kwa sasa ni Kocha Mkuu wa
Real Madrid, kikosi B, lakini ana kesi.
Kesi yake ni madai kwamba
hana vigezo vinavyompa leseni ya kufundisha katika daraja hilo.
Chama cha Makocha cha
Hispania (CENAFE), kimeamsha madai kuhusiana na Zidane na kusisitiza kinataka
kupata uhakika.
Iwapo itabainika kwamba
Zidane hana vigezo sahihi, maana yake Real Madrid itakuwa imekiuka kipengele
namna 104 na adhabu yake ni kufungiwa kuanzia mechi nne hadi 16 au mwezi mmoja
hadi sita.
0 COMMENTS:
Post a Comment