October 21, 2014

Yule mshambuliaji wa timu ya taifa ya Benin aliyeshindwa kufurukuta mbele ya mabeki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani jana amepiga bonge la bao akiichezea timu yake dhidi ya Manchester United.


Stephane Sessegnon amefunga bao hilo kwa shuti kali la kasi ya kilomita 91 kwa saa na kuifanya West Bwrom iongoze kwa bao moja dhidi ya Man United.

Mshambuliaji huyo alitua jijini Dar es Salaam na kuingoza Benin iliyotandikwa kwa mabao 4-0 dhidi ya Taifa Stars.

Bao lake lilikuwa moja ya mabao manne bora kwenye mechi hiyo iliyoisha kwa sare ya bao 2-2.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic