October 2, 2014



Real Madrid imelazimika kufanya kazi ya ziada kushinda kwa mabao 2-1 dhidi ya timu kibonde ya Ludogoret.

Mabao ya Madrid katika mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi yalifungwa na Cristiano Ronaldo kwa mkwaju wa penalti lakini ikiwa ni baada ya kukosa mkwaju wa kwanza, Madrid ilipata mikwaju miwili ya penalti.
Bao la pili na la ushindi lilifungwa na mshambuliaji Mfaransa, Karim Benzema.

Katika mechi nyingine, Atletico Madrid ikiwa nyumbani, imeituliza Juventus ya Italia kwa kuitwanga kwa bao 1-0, muuaji akiwa ni Mturuki, Arda Turan, kama unamkubuka ndiyo yule aliyeiua Real Madrid.

MATOKEO MENGINE LEO:
Zenit 0-0 Monaco
B. Leverkusen 3-1 Benfica
Anderlecht 0-3 Borussia Dortmund
Malmo 2-0 Olimpiakos

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic