October 22, 2014


Kipa kinda wa Simba, Peter Manyika amesema alidaka mechi dhidi ya Yanga kwa presha kubwa ya kutokufungwa kwa kuhofia Baba yake mzazi, Manyika Peter kuhusishwa kama angekosea na kuruhusu bao.


Kinda huyo, alidaka mechi hiyo ikiwa ya kwanza kwenye msimu huu wa Ligi Kuu Bara tangu ajiunge na timu hiyo iliyocheza michezo minne na kutoka sare yote.
MANYIKA PETER, BABA MZAZI WA PETER MANYIKA. HAPA ALIKUWA KAZINI NCHINI OMAN AMBAKO NI KIPA WA MAKIPA WA KIKOSI CHA SEEB.

Alipata nafasi hiyo ya kudaka baada ya makipa wakongwe wa timu hiyo kupata majeraha kwenye sehemu mbalimbali.

 Manyika amesema kuwa kabla ya mechi hiyo mashabiki wengi wa Simba hawakuwa na imani naye wakihofia huenda akafungisha, lakini anashukuru hakufungwa.
 “Nilicheza mechi ya Yanga nikiwa na presha kubwa ya kupoteza mechi ile, kwa sababu nilihofia kufungwa na baadaye kutajwa baba yangu ndiyo chanzo kutokana kuwahi kuidakia timu hiyo.

 “Lakini ninashukuru sikuruhusu bao katika mechi hiyo dhidi ya Yanga, kikubwa mashabiki wanatakiwa kujenga imani na mimi nikiwa golini  tukiwa tunacheza na Yanga,” alisema Manyika.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic