October 24, 2014


Ni furaha kubwa kwa mashabiki wa Simba, baada ya wachezaji wake Emmanuel Okwi na Jonas Mkude kufanya mazoezi jioni hii mjini Mbeya.

Okwi amefanya mazoezi kwenye kikosi cha timu hiyo ambacho kimetua hapo kuivaa Prisons wikiendi.
Awali daktari wa Simba, Yassin Gembe alisema asubuhi Okwi alishindwa kufanya mazoezi.
“Jioni hii Okwi amefanya mazoezi, asubuhi ilikuwa kidogo ana tatizo la enka. Alikimbia lakini baadaye akalazimika kidogo kusubiri nje.
“Ila jioni hii amefanya mazoezi vizuri sambamba na wenzake. Pia Mkude ameanza mazoezi,” alisema Gembe.

Tayari Simba imecheza mechi nne kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na zote imetoka sare.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic