MKATABA WA KIBIASHARA
Leo tarehe 30.Oct.2014, Mbeya City Fc inasaini mkataba wa makubaliano ya
kibiashara na Benki ya Posta Tanzania
(TPB).
Huu ni mkataba wa kibiashara (Siyo udhamini) kwa maana kuwa kupitia kadi
za ATM ambazo mashabikiwa Mbeya City Fc watapewa baada ya kufungua ‘akaunti’
wataweza kuichangia timu kupitia huduma za kibenki watakazokuwa wakizifanya kwa
kutumia akaunti zao.
Mkataba huu pia utaifanya club kufahamu idadi ya mashabiki iliyonao
nchini kote.
DISMAS TEN
AFISA HABARI NA MAWASILIANO
MBEYA CITY COUNCIL FC.
0 COMMENTS:
Post a Comment