Kocha Roberto Martinez wa Everton ameeleza nia yake ya kutaka
kumuongezea mshambuliaji wake Samuel Eto’o ‘shemeji’ mkataba wa mwaka mmoja.
Eto’o, 33, alisaini mkataba wa miezi 12 alipojiunga na timu hiyo Agosti,
mwaka huu.
Lakini Martinez ameonyesha kuridhishwa na kiwango chake na kusema ni mtu
mwenye bahati ya kipaji cha soka kutoka kwa Mungu.
Hata hivyo, Eto’o amepewa masharti ilia pate nafasi hiyo ya kuongezewa
miezi 12.
Anachotakiwa kufanya raia huyo wa Cameroon kwa msimu huu ni kupata
nafasi 15 za kuanza katika kikosi cha
kwanza.
0 COMMENTS:
Post a Comment