October 1, 2014

PLUIJM
Na Mwandishi Wetu
Shirikisho la Soka la Ghana (GFA) limeiagiza klabu ya Berekum Chelsea kumlipa kocha wake wa zamani, Hans van der Pluijm ambaye aliwahi kuinoa Yanga kitita cha dola 215,000 (zaidi ya Sh milioni 361).
Chelsea imetakiwa kumlipa Mholanzi huyo kitita hicho kikubwa cha fedha kutokana na uamuzi wake wa kufanya mambo kienyeji.
Chelsea hiyo ya Ghana ilifanya vziuri kwenye Ligi ya mabingwa Afrika ikiwa na kocha huyo, lakini baadaye wakafikiana kuvunja mkataba.
Lilipofikia suala la malipo, Chelsea wakawa wagumu na kusababisha Pluijm kufungua kesi kwenye shirikisho hilo.
Tayari shirikisho hilo limehibitisha kuidhinisha malipo hayo kwa Pluijm ambaye aliiongoza Yanga kuilaza Al Ahly jijini Dar es Salaam, lakini Yanga ikang’olewa kwa mikwaju ya penalti.
Akizungumza jana na Championi Jumatano kutoka Accra, Ghana, Pluijm alisema kweli hilo limepitishwa na shirikisho hilo, lakini Chelsea wamekataa.
“Wana nafasi ya kukata rufaa, lakini wameishasema ni kiasi kikubwa. Hivyo ninasubiri kwanza, sasa sitaweza kulizungumzia kwa undani,” alisema.
Baada ya hapo, Pluijm aliamua kuodoka kwenda Saudi Arabia akimtwaa na Charles Boniface Mkwasa kwenda kumsaidia kazi katika klabu ya Al Shaollah ya nchini humo.
Hata hivyo, walishindwana na Mholanzi huyo akarejea Ghana ambako ameoa raia wa nchini hiyo na Mkwasa amerudi nyumbani ambako ameula sasa ameajiriwa na TFF.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic