October 24, 2014


Wakati timuatimua ikiendelea ndani ya Ndanda FC, kutokana na mwendo mbovu wa timu, zimeibuka taarifa kuwa sababu kubwa ya kufanya vibaya ni mgogoro wa viongozi ndani kwa ndani na wachezaji kutolipwa stahiki zao.


Taarifa hizo zimeibuka siku chache baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Denis Kitambi na Katibu Mkuu, Edmund Njowoka kutimuliwa.

Habari kutoka ndani ya klabu hiyo zinadai viongozi kwa sasa wapo bize kushughulikia migogoro huku wachezaji wakiwa katika hali ngumu kwa kutolipwa mishahara.

“Jambo baya zaidi ni kuwa, bado kuna wachezaji wanaidai klabu fedha zao za usajili ambazo hawajamaliziwa mpaka leo, ndiyo maana wamekuwa wakicheza chini ya kiwango,” kilisema chanzo.

Katibu Msaidizi wa Ndanda, Suleiman Kachele, alipoulizwa juu ya tuhuma zote hizo, alisema siyo kweli.

Lakini imeelezwa kuna hali ya kutoelewana kati ya viongozi na vionozi, hali inayosababisha mpasuko huo.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic