TAMBWE AKIPAMBANA UWANJANI... |
Kiungo Shabani Kisiga ma Mrundi Amissi Tambwe
ndiyo wataoongoza mashambulizi ya Simba leo mjini Mbeya dhidi ya Prisons.
Simba ambayo iko ugenini Mbeya, iko tayari
kupambana katika mechi yake ya kwana ya ugenini.
Pia inapambana ikitaka ushindi wake wa kwanza
katika Ligi Kuu Bara baada ya kucheza mechi nne nyumbani Dar na kutoka sare
zote.
Kocha Mkuu wa Simba, Mzambia, Patrick Phiri,
amesema Tambwe ataanza au atapewa nafasi kubwa ya kucheza.
Pia kiungo Ramadhani Singano ‘Messi’ ana
nafasi kubwa ya kuanza katika kikosi cha leo.
Tayari mashabiki wameanza kusogea kwenye eneo
la Uwanja wa Sokoine kwa ajili ya mechi hiyo.
Simba inakuwa timu kubwa ya kwanza kucheza
Mbeya tokea kuanza kwa msimu huu.
0 COMMENTS:
Post a Comment