October 21, 2014

YP (KULIA) WAKATI WA UHAI WAKE. HAPA ALIKUWA NA KUNDI LA WANAUME WALIPOTEMBELEA OFISI ZA GLOBAL PUBLISHERS.

Msanii YP aliyekuwa katika kundi la Wanaume TMK amefariki dunia.

YP alikuwa akisumbuliwa na kifua kwa muda mrefu, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Aliyekuwa bosi wake, Said Fella amesema mipango ya mazishi inafanywa kwa kushirikiana na ndugu zake.
Bado haijajulikana kama mwili wa marehemu utapelekwa kwao Mbeya au atazikwa jijini Dar.

YP alichipukia akiwa na msanii mwingine Y Dash ambao waliokuwa chipukizi katika TMK Family kabla ya kusambaratika na kuunda makundi mawili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic