November 24, 2014


Simba na Yanga wiki hii zinatarajia kuingia kambini kujiandaa na mchezo wa Nani Mtani Jembe utakaopigwa Desemba 13, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa. Ikumbukwe Simba ndiyo wenye kombe hilo, ambalo walilitwaa msimu uliopita baada ya kuwanyuka wapinzani wao mabao 3-1, huku straika Amissi Tambwe akitupia mawili.

Hata hivyo, wakati Kocha wa Yanga, Marcio Maximo akitarajia kutia guu nchini leo Jumatatu akitokea kwao Brazil, Tambwe naye anatua Bongo leo akitokea kwao Burundi ambapo alikwenda kwa ajili ya mapumziko mafupi.

Tambwe hapendwi na mashabiki wa Yanga kutokana na mabao yake ya Nani Mtani Jembe iliyopita, kufukuzisha benchi zima la ufundi, lililokuwa chini ya Mholanzi Ernie Brandts pamoja na Fred Felix ‘Minziro’.

Akizungumza na kutoka mjini Bujumbura, Tambwe alisema kuwa ameamua kurejea mapema kwa ajili ya kuwahi mazoezi, tayari kuwavaa Yanga hiyo Desemba 13.

“Mpaka sasa (jana) bado nipo Bujumbura nimepumzika, ila natarajia kuja huko (Dar) Jumatatu (leo) kwa ajili ya kujifua kujiandaa na mchezo unaotukabili,” alisema.

Aidha Ofisa Habari wa Simba, Humphrey Nyasio, alisema wachezaji walitarajiwa kuanza kurejea kuanzia jana kwa wachezaji wote wa kitaifa na kimataifa.


Licha ya Simba kuonekana kutofanya vema, hata hivyo imekuwa na matokeo ya kuridhisha mbele ya Yanga, ambapo mara ya mwisho kwa Yanga kushinda ilikuwa msimu wa 2012/13 huku Simba ikiigaragaza kwenye Mtani Jembe kabla ya kutoa sare kwenye michezo mitatu iliyofuatia ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic