November 1, 2014

KASEJA AKISAINI KUICHEZEA YANGA MBELE YA BIN KLEB (KUSHOTO) ANAYEONEKANA NYUMA NI ABDULFATAH AMBAYE SHUGHULI YA KUSAINI ILIFANYIKA OFISINI KWAKE KARIAKOO JIJINI DAR ES SALAAM.
Kumekuwa na malumbano ya hapa na pale katika ya Menaja wa kipa mkongwe nchini, Juma Kaseja na uongozi wa Yanga.

Meneja huyo, Abdulfatah Saleh amekuwa akisisitiza kuhusiana na suala la mchezaji wake kwamba hajalipwa fedha zake kama ilivyokuwa inatakiwa.
Alieleza siku sahihi iliyotakiwa kulipwa fedha hizo na akasisitiza kufanya hivyo ni kutotekeleza mkataba sahihi.
KASEJA AKISAINI MBELE YA SEIF MAGARI. ANAYEONEKANA NYUMBA NI ABDULFATAH
Lakini akasisitiza suala la mchezaji wake kupata nafasi kwa kuwa anaamini kiwango chake.
Uongozi wa Yanga ulijibu hoja hizo juujuu na kusisitiza kwamba amelipwa lakini Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu akasema hamtambui meneja huyo.
Njovu akasisitiza meneja huyo hatambuliki na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) wala lile la Tanzania (TFF).
ABDULFATAH
Mazungumzo hayo ya uongozi wa Yanga yanaweza yakawa si hoja ya msingi hata kidogo labda kama Njovu atasema ana utani na Abdulfatah kwa kuwa ni mshikaji wake.
Lakini katika ishu muhimu na makini kama hiyo, Yanga hawapaswi kuleta utani badala yake kufanya mambo kwa uhakika na kutimiza ahadi zao inavyotakiwa.
Wanajua hawajamlipa Kaseja, basi wana kila sababu ya kufanya hivyo mara moja kwa kuwa viongozi ndiyo wanaopaswa kuwa watetezi wa wachezaji.
Njovu ndiye mtendaji, hapaswi kuacha mianya ndani ya Yanga, kikubwa amalizane na Kaseja na kupunguza malumbano hayo. Si lahisi meneja wa Kaseja atakurupuka na kuanza kudai mchezaji wake alipwe wakati malipo yaliishafanyika.
Lakini kusema hawamtambui meneja huyo ni jambo jingine la kuchekesha pia. Kama mwenye alivyosema, wakati Kaseja anajiunga na Yanga, alisaini fomu za usajili ofisini kwake.
Ukiziangalia hizo picha Abdulfatah anaonekana nyuma wakati Kaseja akisaini mbele ya mabosi wa Yanga Seif Ahmed ‘Magari’ na Abdallah Bin Kleb.
Maana yake, Abdulfatah ndiye alisimamia mchezo mzima na Yanga wanamtambua. Kama wangekuwa hawamtambui, wasingefika ofisini wake, wasingefanya shughuli ya kusaini ofisini kwake. Hivyo Yanga mjibu hoja za msingi na ikiwezekana mlimalize suala hili kuliko kutaka kulizungusha na mwisho kulikuza.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic