December 20, 2014

DK KALYAN AKIWA NA KIONGERA
Daktari nguli aliyemtibu mshambuliaji wa Simba, Paul Kiongera amewatoa hofu Msimbazi na kuwaambia Mkenya huyo atarejea na kucheza soka.


Dk Hemant Kalyan wa nchini India amesema upasuaji wa Kiongera ulifanyika kwa mafanikio makubwa.

"Kweli daktari ambaye ni bingwa katika upasuaji amethibitisha. Katuambia Kiongera atarejea vizuri," kilieleza chanzo.

Kiongera anatarajia kurejea wiki ijayo baada ya matibabu hayo.

Simba inaendelea kumlipa mshahara mshambuliaji huyo wa zamani wa KCB ya Kenya lakini ilimuondoa kwenye usajili na nafasi yake kuchukuliwa na Mganda, Danny Sserunkuma.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic