December 18, 2014


Kocha Marcio Maximo ameendelea na mazoezi ya kuinoa Yanga.
Kocha huyo amefanya hivyo jana na leo ikiwa ni sehemu ya kuonyesha hatambui suala la kuondolewa kwake kazini.


Ingawa tayari alishafanya mazungumzo na uongozi wa Yanga kuhusiana na hilo, taarifa zinaeleza bado hajakabidhiwa barua rasmi.

Kocha huyo Mbrazil na msaidizi wake, Leonardo Neiva waliendelea na kazi yao kama kawaida kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Loyola.

Tayari Kocha wa zamani wa Yanga, Hans van der Pluijm raia wa Uholanzi yuko jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Mbrazil huyo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic