Mwenyekiti wa zamani wa Simba, Hassan Dalali,
alizua jambo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar katikati ya wiki hii baada ya kugeuka
nyuma wakati beki wa timu hiyo, Nassoro Masoud ‘Chollo’ alipokuwa akijiandaa
kupiga penalti wakati timu yake ilipokuwa ikipambana na Mbeya City.
Simba iliyokuwa nyuma kwa mabao 2-1, ilipata
penalti katika dakika ya 90 na ilitakiwa ikwamishe nyavuni ili kuiokoa timu
hiyo na kipigo, haikuwa hivyo, penalti hiyo iligonga mwamba na kuokolewa na
mabeki wa Mbeya City.
Wakati Chollo akijiandaa kupiga penalti hiyo,
Dalali aligeuka na kuupa uwanja kisogo, huku mashabiki wa Simba wakiwa kimyaa.
Baada ya Chollo kukosa, kiongozi huyo na wenzake wa Simba walijikuta wakiwa wapole
na kuondoka uwanjani hapo kwa kuwa muda huohuo mwamuzi alimaliza mchezo.
0 COMMENTS:
Post a Comment