Timu ya African Sports ya Tanga, inayoshiriki
Ligi Daraja la Kwanza, inahitaji pointi tatu tu kuweza kucheza Ligi Kuu Bara
msimu ujao.
Kwa sasa, African Sports ndiyo vinara wa Kundi
A wakiwa na pointi 41, baada ya juzi Jumatatu kuichapa Majimaji bao 1-0.
Leo Jumatano, African Sports itaumana na JKT
Mlale kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na endapo ikishinda mchezo huo basi
itakuwa imejikatia tiketi ya kucheza ligi kuu msimu ujao kwa kufikisha pointi
44 ambazo katika michezo iliyobaki timu za Majimaji, Friends Rangers na Lipuli
zinaweza kuzifikia lakini haziwezi kuishusha African Sports kutokana na uwiano
mzuri wa mabao ilionao.
Wapenzi wa soka kutoka Tanga wanatamani timu
hiyo ipande ligi kuu ili washuhudie burudani iliyopotea kwa muda mrefu pindi
zinapokutana timu hasimu kutoka jiji hilo za Coastal Union na African Sports.
0 COMMENTS:
Post a Comment