Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi alionyesha mapenzi kwa kipa Ivo Mapunda baada ya kukimbilia kwenda kufunga kamba za viatu vyake.
Okwi alifanya hivyo wakati wa mazoezi ya Simba yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Boko jijini Dar es Salaam.
Makipa wote wa Simba akiwemo Ivo walikuwa wamevaa glavu hivyo haikuwa lahisi kujifunga na Ivo alipoomba msaada, Okwi licha ya kuwa mbali, aliwahi kufika na kumfunga kamba.
"Nitafanya kazi hiyo mimi, wewe tulia," alisema Okwi, akapiga magoti na kuanza kufunga kamba za viatu vya Ivo.
FOOTBAL IS LOVE.
0 COMMENTS:
Post a Comment