January 31, 2015


Mabao mawili aliyofunga Danny Sserunkuma wakati Simba ikiimaliza Ruvu JKT kwa mabao 2-1 leo, amezawadiwa Kocha Goran Kopunovic.


Wachezaji Simba wameamua kumzadia kocha huyo mabao hayo kwa kuwa kesho ni siku yake ya kuzaliwa, anafikisha miaka 48.

Kabla ya mchezo huo, Kopunovic aliwaomba wachezaji hao kumzawadia kitu kizuri kwa ajili ya sikukuu yake ya kuzaliwa.

“Kweli kocha aliwaambia anaomba msaada wao, aliwaambia angependa kusherekea siku yake ya kuzaliwa akiwa na amani.

“Hivyo aliwaomba kuifunga Ruvu JKT ili Wanasimba wafurahi naye awe na amani hiyo kesho.

“Kweli utaona wachezaji wamejituma sana licha ya mechi kubwa ngumu na mwisho wamefanikiwa kushinda na baada ya hapo wamemzawadia mabao hayo mawili ya Sserunkuma,” kilieleza chanzo.


Huo ni mchezo wa tatu wa Kopunovic akiwa na Simba katika Ligi Kuu Bara na amefanikiwa kushinda mechi mbili na kupoteza mmoja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic