January 27, 2015


Washindi wa Copa Coca-Cola 2014 wamekabidhiwa zawadi zao za fedha kutoka kwa mdhamini wa michuano hiyo ya umri chini ya miaka 15 kwa wavulana na wasichana kampuni ya Coca-Cola. Fedha hizo kwa washindi mbalimbali tayari zimeingizwa kwenye akaunti zao.


Kwa upande wa wavulana; washindi na kiwango walichopata ni mabingwa Dodoma (sh. milioni nane), makamu bingwa Kinondoni (sh. milioni tano), mshindi wa tatu Kigoma (sh. milioni tatu) wakati timu yenye nidhamu Tanga (sh. milioni moja).

Mchezaji bora Mwami Ismail kutoka Kigoma (sh. 500,000), mfungaji bora Timoth Timoth wa Dodoma (sh. 500,000), kipa bora Kelvin Deogratia wa Geita (sh. 500,000) na mwamuzi bora Abdallah Mbarome kutoka Zanzibar sh. 500,000).

Kwa upande wa wasichana ni mabingwa Kinondoni (sh. milioni tano), makamu bingwa Ilala (sh. milioni tatu), mshindi wa watatu Temeke (sh. milioni mbili) wakati timu yenye nidhamu Mbeya imepata sh. milioni moja).

Zubeda Mohamed wa Kinondoni ambaye ndiye mchezaji bora amepata sh. 500,000, mfungaji bora Stumai Abdallah wa Temeke sh. 500,000 wakati kipa bora ni Suleta Saad wa Zanzibar sh. 500,000.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic