January 28, 2015


Baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe kuliomba Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kumchukulia hatua straika wa Yanga, Amissi Tambwe kutokana na kumpiga kibao beki wa Ruvu Shooting, George Michael, uongozi wa Yanga umeibuka na kujibu mapigo.


Tambwe na beki huyo waliingia kwenye vita kali kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa katika Uwanja wa Taifa huku awali Tambwe akilalamika kuwa beki huyo alimkaba koo lakini baadaye ikafahamika kuwa naye alimpiga kibao.

Katibu wa Yanga, Dk Jonas Tiboroha, ameishangaa kauli ya Hans Poppe kwa kile alichosema anaingilia mambo yasiyomhusu huku akihoji kama siku hizi amekuwa msemaji wa wanajeshi hao, kazi ambayo ni ya Masau Bwire.

 “Ki ukweli ilinishangaza sana kusikia kauli ya kiongozi wa timu isiyohusika katika tukio kulisemea kuwa Tambwe anatakiwa kufungiwa, ni maajabu sana. Mimi binafsi sijawahi kumsikia kiongozi yeyote wa Yanga akizungumzia timu nyingine, labda iwe na mechi na timu yake na huo ndiyo weledi kitaaluma (professionalism).

“Haiingii akilini hata chembe kusikia kiongozi wa Simba anaibuka na kuzungumzia mchezo usiomhusu hata kidogo, labda aweke wazi kama siku hizi ameajiriwa na Ruvu ili tujue moja,” alisema Dk Tiboroha.

Sakata hilo liliibuliwa na gazeti kiongozi la michezo nchini, Championi lililochapisha picha iliyomuonyesha Michael akimpiga kabali Tambwe huku akivuja damu mdomoni na baadaye kuonyesha nyingine fowadi huyo akijibu mapingo kwa kumpiga beki huyo kofi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic